Monday, October 29, 2012

WIMBO MPYA WA DIAMOND "nataka kulewa" BONYEZA HAPA KUSIKILIZA

HONGERA J4 KWA KUCHUKUA JIKO



J4 akiwa na mwandani wake baada ya kufunga pingu za maisha katika pozi lenye tabasamu la nguvu kwa furaha


Chanda chema huvishwa pete, kwa uzima na ugonjwa mpaka kifo



Wadau wa Augsburg nao waliwakilisha, kutoka kulia Malumbo S Malumbo (mambo bado Sounds), Othman Babu (Black Mamba) bwana harusi na bibi harusi.


Monday, October 22, 2012

CHEGE CHIGUNDA AKANUSHA KUMTIA MIMBA MKE WA MTU



Msanii mwenye jina kubwa ndani ya bongo kutoka mitaa ya Temeke jijini Dar es Salaam leo alifunguka alipokuwa akipiga "story" na kipindi cha XXL cha clouds fm. Chege alikanusha vikali tuhuma au uzushi huo uliokuwa umezagaa kila kona baada ya kubainika kuwa mtu huyo hakuwa na ushahidi sababu ambayo imempelekea Chege kusema kuwa atachukua hatua na taratibu za kisheria dhidi ya mtu huyo


Friday, October 19, 2012

OGOPA DEEJAYZ NDIO WATAKAO HUSIKA KATIKA KUANDAA VIDEO YA WIMBO MPYA WA TUNDA MAN



Msanii kutoka kundi la Tip Top Connection lenye maskani yake maeneo ya Magomeni jiji Dar es Salaam "Tunda Man" leo aliamua kufunguka kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa "Face Book". Tunda aliamua kuwatoa hofu mashabiki wa masongi yake yake kwa kuandika kuwa ngoma mpya tayari imekamilika kwa upande wa sauti na kinachofuata ni video ambayo itafanywa nchini kenya na wakali wa siku wa muziki wa Afrika Mashariki "Ogopa Deejayz". Alimalizia kwa kusema kaeni mkao wa kula, mambo matam na mazuri yanakuja.

Thursday, October 11, 2012

KITENDO CHA DIAMOND KUVUA NGUO ON THE STAGE,... NINI TAFSIRI YAKO???



Gumzo lililopo kwa wadau wengi wa burudani ni kwa sasa ni juu ya kitendo cha msanii wa Bongo Fleva ambaye anashika chati ya juu kwa sasa "Diamond Platnumz" Nassib Abdul kushusha suruali yake mpaka chini na kubaki na nguo ya ndani kisha kuwapa mashabiki mgongo na kuinama.

Habari hii yazungumziwa sana kutokana na baadhi ya wasanii wa Bongo movi kukutwa na matukio kama hayo katika kipindi cha hivi karibuni na kukemewa vikali sana na baadhi ya wasanii wa muziki wa kizazi kipya (bongo fleva). Jumamosi iliyopita katika kilele cha Tamasha la Fiesta jijini Dar es Salaam baadhi ya mashabiki hawakuamini macho yao baada ya msanii Diamond kufanya kituko hicho.

Kila mtu kwa upande wake anazungumzia tofauti kituko hicho, kuna gazeti lilidiriki kuandika eti kuwa amemuiga mpenzi wake wa zamani "Wema sepetu" kwani naye pia aliwahi kupatwa na mkasa kama huo kwa kuonesha baadhi ya sehemu za makalio yake kwenye jukwaa la Fiesta mwka jana. Pia kuna waliosema kuwa labda anamuiga afande sele kwani pia aliwahi kufanya kituko kama hicho miaka kadhaa iliyopita katika ukumbi wa Diamond Jubilee. Na kuna mdau aliyeandika kwenye ukurasa wake wa face book " ah Diamond kama 50 cent"

JE WEWE MDAU TAFSIRI YAKO NINI???


HUYU JAMAA ANAUCHUNGU NA YANGA KULIKO HATA WEWE

Tuesday, October 9, 2012

Friday, October 5, 2012

MASIKINI LULU!!!! ARUDISHWA TENA LUPANGO NA KESI YAKE YAANZA UPYA




Elizabeth Michael (LULU)

Akiwa chini ya ulizi wa jeshi la polisi na kuhifadhiwa rumande kwa miezi kadhaa kutokana na tuhuma zinazomkabili za kusababisha kifo cha msanii mwenzie Steven Charles Kanuma. Msanii "lulu" leo alijikuta katika wakati mgumu baada ya mahakama ya rufaa kuamua kuwa kesi yake irudishwe mahakama ya kisutu na kuanza kusikilizwa upya kutokana na kutofuatwa kwa baadhi ya taratibu, ambapo Naibu msajili wa mahakama ya rufaa Bi Zahra Marume alitoa ufafanuzi huo masaa machache yaliyopita wakati kesi hiyo ilitarajiwa kusikilizwa na kushindikana. 

HUYU JAMAA MZIMA KWELI HUYU????